Thursday, December 29, 2016

MESSI NI BORA KULIKO RONALDO - RAFINHA.

LIONEL Messi anaweza kuwa amemaliza wa pili mbele ya Cristiano Ronaldo katika tuzo za Ballon d’Or, lakini mchezaji mwenzake wa Barcelona Rafinha hana shaka kabisa kuwa nyota huyo wa kimataifa wa Argentina ndio bora duniani. Ronaldo alishinda tuzo hiyo akiwashinda Messi na nyota wa Atletico Madrid Antoine Griezmann. Lakini Rafinha mwenye umri wa miaka 23 anaamini Messi anastahili kupewa heshima ya kuwa bora kuliko wachezaji wote wa sasa. Akihojiwa Rafinha amesema kwa upande wake mchezaji bora duniani ni Messi.

No comments:

Post a Comment