Thursday, December 29, 2016

OFA YA CHELSEA KWA KESSIE YAGONGA MWAMBA.

WAKALA wa Franck Kessie amedai kuwa ofa ya euro milioni 25 iliyotolewa na Chelsea kwa ajili ya kiungo huyo imekataliwa na Atalanta. Chelsea wanataka kutafuta mbadala wa Oscar ambaye wamemuuza China, katika kipindi cha usajili wa dirisha dogo Januari mwakani. Kessie amefunga mabao sita katika mechi 16 alizocheza msimu huu na kuisaidia Atalanta kukwea mpaka nafasi ya sita katika msimamo wa Serie A. Kiungo huyo mwenye umri wa miaka 20 amekuwa katika kiwango kizuri msimu huu na kupelekea kufananishwa na nyota mwenzake wa kimataifa wa Ivory Coast Yaya Toure, na wakala wake George Atangana amesema Chelsea watakabiliwa na upinzani katika kuwania saini yake. Atangana amesema wamekuwa wakipata ofa nyingi kutoka Ligi Kuu kwa klabu kama Chelsea, Liverpool, Manchester City, Manchester United na Arsenal. Wakala huyo aliendelea kudai kuwa hawezi kusema thamani halisi ya mteja wake lakini wanazungumzia mmoja kati ya wachezaji bora kabisa chipukizi.

No comments:

Post a Comment