Thursday, December 29, 2016

MARTIAL MGUU NDANI MGUU NJE UNITED.

WAKALA wa Anthony Martial amesema yeye pamoja na mteja wake wanafuatilia kwa karibu ofa kutoka Sevilla kipindi hiki ambacho chipukizi huyo wa Manchester United anapanda mustakabali wake. Martial mwenye umri wa miaka 21 alitokea katika benchi na kucheza dakika 16 pekee katika ushindi wa mabao 3-1 waliopata United dhidi ya Sunderland Desemba 26, huku akiwa ameanza katika mechi moja pekee kati ya nne zilizopita. Nyota huyo wa kimataifa wa Ufaransa amekuwa akipata tabu kupata nafasi katika kikosi cha Jose Mourinho msimu huu na kutakiwa na meneja huyo kujituma ili aweze kupata nafasi ya kuanza mara kwa mara. Pamoja na taarifa kuwa United bado wanataka kuendelea kubaki na Martial lakini wakala wake Philippe Lamboley amedai kuwa Sevilla wanataka kumsajili mshambuliaji huyo kwa mkopo. Lamboley amesema wanaifuatilia Sevilla kwa karibu kwani ni klabu nzuri, iliyopo nafasi ya nzuri katika La Liga na wapo katika michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya. Mapema wiki hii Mourinho alimtaka Martial kufuata nyayo za mchezaji mwenzake Henrikh Mkhitaryan kama anataka kurejea katika kikosi cha kwanza cha United.

No comments:

Post a Comment