Friday, December 30, 2016

BAADA YA KUFANYA KUFURU KWA TEVEZ, CHINA SASA WAMTAKA RONALDO.

WAKALA Jorge Mendes amedai kuwa Real Madrid ilipewa ofa ya kitita cha paundi milioni 250 kutoka katika klabu moja ya China kwa ajili ya Cristiano Ronaldo. Mendes amesema nahodha huyo wa kimataifa wa Ureno mwenye umri wa miaka 31 hakuwa na mpango na dili hilo ambalo lingemuwezesha kulipwa kiasi cha zaidi ya paundi milioni 85 kwa mwaka. Novemba mwaka huu Ronaldo amesema anaweza kucheza kwa miaka mingine 10 baada ya kusaini mkataba mpya na Madrid ambao unamalizika Juni 2021. Akihojiwa Mendes amesema soko la China ni jipya na wanaweza kununua wachezaji wengine lakini haitawezekana kumnunua Ronaldo. Wakala huyo aliongeza kuwa Ronaldo ni mchezaji bora duniani hivyo ni kawaida kwa ofa kama hizo kuja mara kwa mara. Chini ya ofa hiyo anayodai Mendes, Ronaldo angeweza kulipwa kitita cha paundi milioni 1.6 kwa wiki.

No comments:

Post a Comment