Sunday, December 25, 2016

VINCENT BOSSOU AITWA TOGO KWA AJILI YA AFCON.

BEKI mahiri wa klabu ya soka ya Yanga, Vincent Bossou ameitwa katika kikosi cha awali cha timu ya taifa ya Togo kwa ajili ya michuano ya Mataifa ya Afrika itakayofanyika huko nchini Gabon mapema mwezi ujao. Beki huyo amekuwa muhimili mkubwa katika safu ya ulinzi ya Yanga toka asajiliwe na kufanikiwa kuliziba vyema pengo la nahodha wa klabu hiyo Nadir Harub ambaye majeruhi ya mara kwa mara yamemfanya kupoteza nafasi yake katika kikosi cha kwanza. Wengine walioitwa katika kikosi hicho ni beki Yaovi Joseph Douhadji ambaye anacheza katika klabu ya Rivers United inayoshiriki Ligi Kuu ya Nigeria. Mshambuliaji mkongwe wa nchi hiyo Emmanuel Adebayor naye ameitwa na kocha Claude Leroy pamoja na kutokuwa na timu yeyote hivi sasa baada ya kuondoka West Ham.

No comments:

Post a Comment