Sunday, December 25, 2016

MESSI NI BORA KULIKO RONALDO - GUARDIOLA.

MENEJA wa zamani wa Barcelona, Pep Guardiola amesisitiza kuwa hakuna mjadala wowote pindi unapokuja wakati wa kuamua nani zaidi kati ya Lionel Messi na Cristiano Ronaldo. Ronaldo alitwaa tuzo ya Ballon d’Or mwaka jana baada ya kuwa na mwaka mzuri ambao walitwaa taji la Ligi ya Mabingwa Ulaya na Euro 2016, lakini Guardiola amedai kuwa Ronaldo bado ana safari ndefu ya kumfikia Messi. Hivi karibuni meneja wa Barcelona Luis Enrique alidai kuwa ni jambo la kijinga kumfananisha Messi na wachezaji wengine jambo ambalo linaungw amkono na Guardiola. Akihojiwa meneja huyo wa Manchester City amesema anakubaliana na Enrique kwamba Messi ndio bora, kwani anajua jinsi ya kucheza, kufunga na kuwachezesha wenzake pia jamboa ambalo ni nadra kupata kwa wachezaji wengine. Guardiola aliendelea kudai kuwa kwa heshima kubwa aliyonayo kwa wachezaji wote pamoja na Ronaldo, lakini anadhani Messi yuko katika kiwnago cha juu zaidi.

No comments:

Post a Comment