Sunday, December 25, 2016

JUVENTUS YAPATA PIGO LINGINE KTK SAFU YAKE YA ULINZI.

KLABU ya Juventus, imethibitisha kuwa beki wake Alex Sandro alipata majeruhi ya msuli katika mchezo wa Supercoppa Italiana waliofungwa na AC Milan. Nyota huyo wa kimataifa wa Brazil alitolewa nje na nafasi yake kuchukuliwa na Patrice Evra baada ya dakika ya 33 kwenye mchezo huo uliofanyika jijini Doha, Qatar Ijumaa iliyopita ambapo Milan walishinda kwa changamoto ya mikwaju ya penati 4-3 baada ya kutoka sare ya bao 1-1 katika muda wa kawaida. Sandro anaongeza idadi ya majeruhi katika safu ya ulindi ya Juventus baada ya Leonardo Bonucci na Dani Alves, huku Andrea Barzagli akiwa ndio amerejea hivi karibuni baada ya kukaa nje kwa kipindi cha wiki sita. Mabingwa hao wa Italia hawajatoa muda kamili haswa wa atakaokaa nje beki huyo lakini taarifa kutoka nchini Italia zimedai kuwa atakaa nje kwa wiki sita.

No comments:

Post a Comment