Sunday, December 25, 2016

DEFOE HAENDI KOKOTE - MOYES.

KLABU ya West Ham United imekuwa ikihusishwa na tetesi za kumuwania Jermain Defoe lakini meneja wa Sunderland David Moyes anadaiwa kutokuwa na mpango wowote wa kumuacha mshambuliaji huyo. Sunderland wanashika nafasi ya 18 katika msimamo wa Ligi Kuu huku Defoe ndio akiwa tegemeo la kuwaokoa washishuke daraja. Defoe amefunga mabao nane msimu huu hatua ambayo imefanya kuivutia klabu yake hiyo ya zamani. Akihojiwa kuhusiana na tetesi hizo, Moyes amesema Defoe hauziki kwani ni mchezaji muhimu sana katika kikosi chake. Sunderland watavaana na Manchester United kesho katika mchezo wa Ligi Kuu utakaofanyika katika Uwanja wa Old Trafford.

No comments:

Post a Comment