Sunday, December 25, 2016

RAIS WA VALENCIA AWAOMBA RADHI MASHABIKI.

RAIS wa Valencia, Layhoon Chan ametuma video ya ujumbe wa Christmas akiwaomba radhi mashabiki wa klabu hiyo kufuatia kufanya vibaya kwa timu hiyo mwaka 2016. Valencia wanashika nafasi ya 17 katika msimamo wa La Liga hivi sasa huku Cesare Prandelli akiwa kocha wa tatu kubadilishwa kwa mwaka huu. Klabu hiyo ilianza mwaka na Gary Neville ambaye alitimuliwa Machi na nafasi yake kuchukuliwa na Pako Ayestaran aliyedumu mpaka Septemba na timu hiyo kuchukuliwa na kocha wa muda Voro kabla ya ujio wa Prandelli Octoba. Katika video hiyo Chan aliomba mashabiki kwa msimu mbaya na kuahidi kuwa watajifunza kutokana na makosa na kufanya kazi kwa bidii ili kuhakikisha wanarejesha furaha tena katika klabu hiyo.

No comments:

Post a Comment