Saturday, December 24, 2016

DRAXLER RASMI PSG.

KLABU ya Wolfsburg imethibitisha kuondoka kwa Julian Draxler kwenda Paris Saint-Germain-PSG, huku nyota huyo wa kimataifa wa Ujerumani akisaini mkataba wa miaka minne na nusu na mabingwa hao wa Ligue 1. Taarifa zinadai kuwa PSG wamelipa kitita cha euro milioni 35 kwa ajili ya nyota huyo na wanaweza kulipa ziada ya euro milioni 10 kulingana na mafanikio ya nyota huyo. Wolfsburg imethibitisha katika taarifa yake kuwa tayari wameshafikia makubaliano na PSG na kinachosubiriwa vipimo vya afya. Draxler amejiunga na Wolfsburg kutoka Schalke Agosti waka 2015 lakini amekuwa akipata wakati mgumu kuzoea mazingira pale Volkswagen Arena.

No comments:

Post a Comment