Saturday, December 24, 2016

FIFA KUJA NA SHERIA KALI KUDHIBITI TABIA ZA WACHEZAJI.

KOCHA na mchezaji wa zamani wa kimataifa wa Uholanzi, Marco van Basten amesema Shirikisho la Soka Duniani-FIFA linajadili kama waruhusu nahodha pekee kuzungumza na mwamuzi. Kama hatua hiyo ikiafikiwa itakuwa imelifanya soka kufanana na raga ambapo wana sheria kali kuhusiana na mawasiliano katika mchezo. Van Basten ambaye ni ofisa wa FIFA kitengo cha maendeleo ya kiufundi, amesema kumekuwa na mjadala wa jinsi gani ya kudhibiti tabia za wachezaji na heshima kwa waamuzi. Nguli huyo amesema kumekuwa na wachezaji wengi hivi sasa wanaolalamika wakati wa mchezo, jambo ambalo wanataka kulidhibiti.

No comments:

Post a Comment