Saturday, December 24, 2016

SENEGAL KUWEKA KAMBI YA AFCON CONGO.

KIKOSI cha timu ya taifa ya Senegal kinatarajiwa kucheza mechi mbili za kirafiki kwa ajili ya kujiwinda na michuano ya Mataifa ya Afrika nchini Congo, ambapo ndio wamepanga kuweka kambi yao kabla ya kwenda Gabon. Mechi ya kwanza inatarajia kuwa dhidi ya Libya Januari 8 katika Uwanja wa Kinkele jijini Brazzaville kabla ya kuja kucheza na wenyeji wao katika uwanja huohuo siku tatu baadae. Senegal, ambao bado hawajataja kikosi chao watajiandaa kwa ajili ya michuano hiyo nchini Congo ambayo inapakana na gabon, kuanzia Januari 5. Baada ya kucheza mechi yao ya pili ya kirafiki wataondoka Brazzaville kwenda Franceville ambapo ndio kambi ya kundi B yenye timu za Algeria, Tunisia na Zimbabwe.

No comments:

Post a Comment