Saturday, December 24, 2016

RANIERI APONDA UAMUZI WA FA KUHUSU KADI YA VARDY.

MENEJA wa Leicester City, Claudio Ranieri ameponda uamuzi wa kutupilia mbali rufani ya klabu hiyo kupinnga kadi nyekundu na anadhabu ya kufungiwa mechi tatu aliyopewa mshambuliaji Jamie Vardy. Vardy, mfungaji bora wa Leicester msimu uliopita, alilimwa kadi nyekundu y moja kwa moja katika sare ya mabao 2-2 waliyopata dhidi ya Stoke City na anatarajiwa kaunza kutumikia adhabu yake Jumatatu katika wakati timu hiyo itakapovaana na Everton. Akihojiwa Ranieri amesema kila mtu Uingereza na duniani kote aliangalia lile tukio lakini wote waliona hakuna kibaya kilichofanywa na vardy. Ranieri aliendelea kudai kuwa walikata rufani wakiamini walikuwa na haki na wamesikitishwa na matokeo waliyopata kwani wakati wakifanya makosa au awachezaji wakifanya makosa huwa hawakati rufani.

No comments:

Post a Comment