Saturday, December 24, 2016

MAN UNITED IMEPOTEZA UTAMADUNI WAKE - MOYES.

MENEJA wa klabu ya Sunderland, David Moyes amedai kuwa utamaduni kwa kipindi kirefu uliokuwepo Manchester United sasa umetoweka. Meneja huyo raia wa Scotland alitimuliwa United mwaka 2014 kabla ya kumaliza msimu baada ya kuchaguliwa kuchukua nafasi ya Sir Alex Ferguson. Moyes amesema ilikuwa utamaduni wa klabu hiyo kuchagua mameneja raia wa Uingereza na kamwe hawakuona umuhimu wa kujiingiza katika usajili. Meneja huyo aliendelea kudai kuwa hivi sasa United imebadilika lakini ndio jinsi walivyoamua kwenda. United imetumia kiasi cha paundi milioni 480 toka Ferguson alistaafu mwaka 2013 baada ya kuiongoza timu hiyo kwa miaka 26.

No comments:

Post a Comment