Saturday, December 24, 2016

NFF YAMUOMBA AMOKACHI USHAHIDI KUFUATIA TUHUMA ALIZOTOA.

NAHODHA wa zamani wa Nigeria, Daniel Amokachi amesema desturi ya makocha wazawa kuhongwa ili kuita wachezaji katika timu ya taifa ni jambo la kawaida. Pamoja na kuwa hakuna kocha yeyote alitekutwa na hatia kufuatia tuhuma hizo, kumekuwa na tetesi hizo kwa kipindi kirefu nchini Nigeria. Akihojiwa Amokachi amesema mawakala mara zote wamekuwa wakitoa fedha ili wachezaji wao waitwe katika kambi ya timu ya taifa. Shirikisho la Soka la Nigeria-NFF limemtaka Amokachi kutoa ushahidi kufuatia tuhuma hizo alizotoa. Amokachi mwenye umri wa miaka 43 ambaye alishinda taji la michuano ya Mataifa ya Afrika akiwa mchezaji mwaka 1994, amesema anadhani ni muda wa watu kuongea kuhusu suala hilo ambalo limekuwa likitafuna soka la Nigeria kwa muda.

No comments:

Post a Comment