Friday, January 27, 2017

BARCELONA NA ATLETICO KUKUTANA NUSU FAINALI KOMBE LA MFALME.

MABINGWA watetezi Barcelona wanatarajiwa kupambana na Atletico Madrid katika nusu fainali ya michuano ya Kombe la Mfalme, huku Alaves wakikwaana na Celta Vigo waliowaondosha Reak Madrid katika mashindano hayo. Baada ya kuindosha Real Sociedad katika robo fainali, Barcelona watasafiri kuifuata Atletico katika uwanja wao wa Vicente Calderone kwa ajili ya mchezo wa mkondo wa kwanza Februari mosi kabla ya kurudiana tena katika Uwanja wa Camp Nou wiki moja baadae. Akizungumzia ratiba hiyo, kiungo wa Barcelona Serge Roberto amesema wanakutana na Atletico kwa mara nyingine wanawafahamu vyema hivyo anadhani utakuwa mchezo mgumu. Kiungo huyo aliongeza kuwa makosa kidogo yanaweza kuweka tofauti katika mechi kama hizo.

No comments:

Post a Comment