Monday, January 30, 2017

KIPA WA KAGERA SUGAR AFARIKI DUNIA GHAFLA.

KIPA wa timu ya Kagera Sugar David Burhan amefariki dunia mapema leo katika hospitali ya Bugando, Mwanza baadaya kuugua kwa muda mfupi. Kipa huyo ambaye ni mtoto wa mshambuliaji wa zamani wa Pan AfrikaAbdallah Burhan, aliugua ghafla wakati wakiwa njiani kuelekea Singida kwa ajili ya mchezo wa Azam Federation Cup (FA). Kocha wa Kagera Sugar, Mercy Mexime alithibitisha taarifa hizo na kuongeza kuwa Burhan alianza kuugua wakati wakielekea Singida lakini baadae alipata nafuu kabla ya hali yake kubadilika tena na kulazimika kulazwa Biharamulo kabla ya kuhamishishwa kupelekwa hospitali ya mkoa wa Kagera. Mexime aliendelea kudai kuwa mara baada ya kupata vipimo kipa huyo alipewa rufaa kwenda hospitali ya Bugando ambapo uongozi wa klabu hiyo ulimfanyiwa utaratibu wa haraka wa kumchukulia ndege kwenda Mwanza ambapo alifika jana kuanza matibabu kabla ya kufariki dunia mapema leo. Burhan alijiunga na Kagera Sugar msimu huu akitokea Maji Maji ya Songea, ambayo nayo ilimtoa Mbeya City.

No comments:

Post a Comment