Monday, January 30, 2017

BARCELONA WATAKA GOAL-LINE TECHNOLOGY LA LIGA.

KLABU ya Barcelona imetaka kuanza kutumika kwa mfumo wa kompyuta katika mstari wa goli kwenye La Liga baada ya kukataliwa bao lao la wazi katika sare ya bao 1-1 waliopata katika mchezo dhidi ya Real Betis jana. Baada ya Betis kupata bao la kuongoza katika kipindi cha pili kupitia kwa Alex Alegria, Barcelona walidhani wamesawazisha bao hilo wakati Aissa Mandi alipojaribu kuokoa mpira wa Jordi Alba ambao ulikuwa umevuka mstari. Hata hivyo mwamuzi Hernandez Hernandez hakulikubali bao hilo ingawa picha za video za marudio zilizonyesha wazi mpira ukiwa umetinga wavuni. Meneja wa Barcelona Luis Enrique alikataa kuwalaumu waamuzi kwa kukaa bao lile na badala yake ametaka kuletwa kwa teknologia hiyo ili kuwasaidia katika baadhi ya maamuzi.

No comments:

Post a Comment