Monday, January 30, 2017

WENGER AKANUSHA KUMUWANIA BENZEMA.

MENEJA wa Arsenal, Arsene Wenger amekanusha taarifa zilizozagaa kuwa klabu hiyo inamuwania mshambuliaji wa Real Madrid Karim Benzema. Nyota huyo wa kimataifa wa Ufaransa kwa kipindi kirefu amekuwa akihusishwa na tetesi hizo, lakini Wenger anaamini tetesi zinakuja kwasababu ya utaifa wake. Akizungumza na wanahabari Wenger amesema kwasasa safu yake ya ushambuliaji imekamilika na haoni nafasi ya kuongeza mshambuliaji mwingine. Wenger aliendelea kudai kuwa ana kikosi kikubwa na anaamini kilichokamilika hivyo haoni sababu ya kununua mshambuliaji.

No comments:

Post a Comment