Monday, January 30, 2017

CHAPECOENSE WASHINDA MECHI YAO YA KWANZA.

KLABU ya Chapecoense imefanikiwa kushinda mechi yake ya kwanza toka wachezaji wengi wafariki katika ajali ya ndege Novemba 29 mwaka jana. Watu 71, wakiwemo wachezaji 19 na viongozi walifariki dunia wakati timu hiyo ya Brazil ikisafiri kwenda Colombia kwa ajili ya mchezo wao wa fainali ya Copa Sudamericana. Toka wakati huo klabu hiyo imesajili wachezaji 22 wapya na kuteua meneja mpya. Katika mchezo huo Chapecoense iliwafunga Inter de Lages kw amabao 2-1 katika mashindano ya jimbo ambayo walishinda msimu uliopita, huku mabao yakifungwa na Niltinho na Wellington Paulista. Hiyo inakuwa mechi yao ya pili ya mashindano toka kutokee kwa ajali hiyo ambayo imeacha simanzi kubwa.

No comments:

Post a Comment