Monday, January 30, 2017

BECKHAM ADAI ALIKATAA KWENDA BARCELONA KWA AJILI YA MADRID.

KIUNGO wa zamani wa Manchester United, David Beckham amebainisha jinsi gani klabu ilipofikia makubaliano ya uhamisho wake kwenda Barcelona wakati alipohamia Real Madrid mwaka 2003. Baada ya kutwaa mataji sita ya Ligi Kuu na moja la Ligi ya Mabingwa Ulaya, Beckham aliachana na United na kujiunga na Madrid kwa kitita cha euro milioni 35. Lakini beckham amesema kuwa United walikuwa tayari wameshaafikiana na Barcelona ingawa baadae aligoma kwasababu alikuwa akitaka kwenda Madrid. Akizungumza na kituo kimoja cha redio cha BBC, Beckham amesema ingawa alikuwa na hasira kwa wakati ule kwa jinsi United walivyotaka kumfanyia lakini hakuwahi kuwa na nia yeyote ya kulipiza kisasi. Beckham aliendelea kudai alichukizwa na kitendo kile cha kufanywa mambo bila yeye mwenyewe kujua wakati ndio kwanza walikuwa wametoka kushinda taji la Ligi Kuu.

No comments:

Post a Comment