Monday, January 30, 2017

ELNENY KUIKOSA NUSU FAINALI YA AFCON.

KIUNGO wa kimataifa wa Misri na klabu ya Arsenal, Mohamed Elneny anatarajiwa kukaa nje katika mchezo wa nusu fainali ya michuano ya Mataifa ya Afrika dhidi ya Burkina Faso keshokutwa kutokana na majeruhi. Nyota huyo mwenye umri wa miaka 24 bado anajiuguza majeruhi ya misuli ya kigimbi amayo ilimfanya kukosa pia mchezo wa robo fainali walioshinda bao 1-0 dhidi ya Morocco jana usiku. Kocha wa Misri Hector Cuper amesema Elneny bado anasumbuliwa na majeruhi na wanatarajia kutuma vipimo kwa klabu yake huku wakitumaini ataweza kupona na kucheza kama wakitinga hatua ya fainali. Misri wanatarajiwa kuchuana na Burkina Faso katika mchezo wa nusu fainali utakaochezwa katika mji wa Libreville.

No comments:

Post a Comment