Friday, January 27, 2017

KLABU ZA UINGEREZA ZAWEKA REKODI MPYA KATIKA USAJILI.

KLABU za Uingereza kwa mara nyingine zimeweka rekodi mpya kwa fedha walizotumia katika usajili msimu huu. Jumla klabu zote za soka zimetumia paundi bilioni 3.8 kwa mwaka 2016 ikiwa ni ongezeko la asilimia 14.3 kulinganisha na mwaka 2015. Asilimia 82 ya kiasi chote kimetumiwa na nchi wanachama wa Shirikisho la Soka la Ulaya-UEFA, lakini Uingereza ndio wanaongoza orodha hiyo. Mwaka jana kulishuhudiwa Paul Pogba akijiunga na Manchester United kwa kitita cha paundi milioni 89, wakati wachezaji kama Eric Bailly, Henrikh Mkhitaryan, Leroy Sane, John Stones, Granit Xhaka, Shkodran Mustafi na N’Golo Kante pia wakinunuliwa kwa bei kubwa. Klabu za Ligi Kuu ya Uingereza pekee zimetumia jumla ya paundi bilioni 1.03 mwaka jana ikiwa ni karibu nusu ya fedha zilizotumika kwa klabu zingine tano kubwa Ulaya.

No comments:

Post a Comment