Friday, January 27, 2017

SHANGHAI FA YAKANUSHA TAARIFA ZA ROONEY KUWINDWA CHINA.

CHAMA cha Soka cha Shanghai-SFA kimekanusha taarifa kuwa klabu za Shenhua na SIPG kutuma ofa kwa ajili ya kumuwania nahodha wa Manchester United Wayne Rooney. Rooney mwenye umri wa miaka 31 ambaye ni mfungaji bora wa wakati wote wa United amekuwa akihusishwa na tetesi za kuhamia China baada ya meneja Jose Mourinho kubainisha kuwa hajamzuia nahodha huyo kama atataka kuondoka. Shenhua tayari imeshwanasa Carlos Tevez, Obafemi Martin, Fredy Guarin na Giovanni Moreno na sasa walikuwa wakihusishwa na tetesi za kumuhitaji Rooney pia. Hata hivyo, SFA imetupilia mbali tetesi hizo na kusisistiza klabu hizo haziwezi kufanya hivyo kutokana na sheria zinazidhibiti idadi ya wachezaji wa kigeni wanaopaswa kucheza katika kila mchezo. Sheria mpya iliyotolewa kwa Ligi Kuu ya China, klabu zinapaswa kutumia wachezaji wa kigeni wasiozidi watatu katika kila mchezo.

No comments:

Post a Comment