Wednesday, January 25, 2017

RONALDO ALAMBA TUZO NYINGINE.

MSHAMBULIAJI nyota wa Real Madrid, Cristiano Ronaldo ametunukiwa tuzo nyingine kwa mafanikio aliyopata mwaka 2016. Nyota huyo mwneye umri wa miaka 31, alishinda tuzo ya Ballon d’Or na tuzo ya mchezaji bora wa mwaka wa FIFA baada ya kushinda taji la Ligi ya Mabingwa Ulaya, UEFA Super Cup na Klabu Bingwa ya Dunia akiwa na Madrid pamoja Euro 2016 akiwa na Ureno. Ronaldo sasa ametwaa tuzo ya Mchezaji Mwenye Thamani Zaidi-MVP inayotolewa na Dongquidi, mtandao wa China unaomilikiwa na kampuni ya Suning Group, ambao ni wamiliki wa klabu ya Inter Milan. Nyota huyo wa zamni wa Manchester United ambaye amekuwa mchezaji soka wa kwanza kutajwa katika orodha za kugombea tuzo ya mwanamichezo bora wa mwaka, aliwahsukuru mashabiki waliomchagua na kushinda tuzo hiyo.

No comments:

Post a Comment