Wednesday, January 25, 2017

KALOU ASTAAFU SOKA LA KIMATAIFA.

MSHAMBULIAJI wa Ivory Coast, Solomon Kalou ametangaza kustaafu soka la kimataifa baada ya mabingwa hao watetezi kuenguliwa mapema katika michuano ya Mataifa ya Afrika jana. Akizungumza na wanahabari mara baada ya kikosi chao kuchapwa bao 1-0 na Morocco, Kalou amesema anedhani wakati umefika wa yeye kupisha vijana wengine kutokana na umri wa miaka 31 aliofikia. Kalou aliendelea kudai kuwa hizo zimekuwa fainali zake za sita na amefanikiwa kufika fainali moja na kushinda mara moja. Nyota huyo ambaye kwasasa anakipiga katika klabu ya Hertha Berlin ya Ujerumani amesema kipindi hiki mambo hayakwenda sawa lakini kuna wachezaji chipukizi kama Franck Kessie na Wilfried Zaha ambao anadhani ndio hazina ya taifa hilo katika soka baadae.

No comments:

Post a Comment