Wednesday, January 25, 2017

MKATABA MPYA WAMFANYA COUTINHO KUWA MCHEZAJI ANAYELIPWA ZAIDI LIVERPOOL.

KIUNGO Philippe Coutinho amesaini mkataba mpya na Liverpool ambao utamuweka hapo mpaka mwaka 2022 na kumfanya kuwa mchezaji anayelipwa zaidi na klabu hiyo kwasasa. Uamuzi wa nyota huyo mwenye umri wa miaka 24 kusaini mkataba huo mpya na klabu hiyo mapema leo na kuzima tetesi za kuwaniwa na klabu za Barcelona na Paris Saint-Germain-PSG. Akizungumza na tovuti na klabu hiyo, Coutinho amesema amefurahi kusaini mkataba huo na kuishukuru klabu hiyo pamoja na mashabiki kwa kumfanya kujisikia yuko nyumbani. Nyota huyo aliendelea kudai kuwa atajitahidi kufanya kazi kwa bidii ili kulipa wema na imani kubwa iliyoonyeshwa kwake.

No comments:

Post a Comment