Tuesday, January 24, 2017

SUNDERLAND WAMCHUKUA LESCOTT.

KLABU ya Sunderland imefanikiwa kukamilisha usajili wa Joleon Lescott aliyekuwa mchezaji huru kwa mkataba mfupi wa mpaka mwishoni mwa msimu huu. Nyota huyo wa kimataifa wa Uingereza amekuwa bila timu toka mkataba wake ulipositishwa na AEK Athens Novemba mwaka jana na ameitwa Sunderland ili kuiokoa isishuke daraja. Lescott ambaye amewahi kushinda taji la Ligi Kuu akiwa na Manchester City katika vipindi viwili tofauti, amekuwa akifanya majaribio na Sunderland wakati meneja David Moyes akijipanga kuongeza nguvu safu ya ushambuliaji. Moyes amewahi kumfundisha Lescott wakati wote wakiwa Everton na sasa anaungana na wachezaji wenzake wa zamani wa klabu hiyo akiwemo Steven Pienaar na Victor Anichebe waliopo katika kikosi cha Sunderland.

No comments:

Post a Comment