Tuesday, January 24, 2017

KOCHA WA ALGERIA AJITOA KAFARA BAADA YA KUTOLEWA AFCON.

KOCHA wa timu ya taifa ya Algeria, Goorges Leekens amejiuzulu wadhifa wake huo kufuatia kikosi chake kutolewa mapema katika michuano ya Mataifa ya Afrika. Algeria wanajulikana kwa jina la utani kama Mbweha wa Jangwani walikuwa wakipewa nafasi kubwa katika michuano hiyo lakini walijikuta wakienguliwa jana usiku baada ya kushindwa kupata ushindi wowote huko Gabon. Leekens aliiambia tovuti ya Shirikisho la Soka la nchi hiyo kuwa ameamua kuchukua uamuzi huo kwa faida ya wote. Kocha huyo alimalizia kwa kuitakia timu hiyo mafanikio katika mshindano yote yajayo.

No comments:

Post a Comment