Tuesday, January 24, 2017

TOURE AWAPONDA NYOTA WENZAKE WANAOKIMBILIA CHINA.

KIUNGO wa Manchester City, Yaya Toure amewaponda wachezaji wenzake ambao wanakimbilia China, akidai kuwa angependelea zaidi kufuata nyayo za mshambuliaji wa Manchester United Zlatan Ibrahimovic na kubaki katika ligi yenye ushindani. Klabu za Ligi Kuu ya China zimewanasa nyota kadhaa wenye majina makubwa hivi karibuni akiwemo kiungo wa kimataifa wa Brazil na Chelsea Oscar aliyenunuliwa kwa kitita cha euro milioni 60 na klabu ya Shanghai SIPG. Mahasimu wa SIPG, klabu ya Shanghai Shenhua wao wamemsajili nyota wa kimataifa wa Argentina Carlos Tevez kwa kitita cha euro milioni 84, lakini Toure amesema kwake pesa sio kila kitu. Akizungumza na wanahabari Toure amesema yeye kwa upande wake hachezi soka ili apate pesa bali anacheza kwasababu anafurahia mchezo huo.

No comments:

Post a Comment