Monday, January 23, 2017

AFCON 2016: BAADA YA KUIFUNGISHA VIRAGO ALGERIA, SENEGAL SASA KUIVAA CAMEROON.

TIMU ya taifa ya Algeria imeenguliwa katika michuano ya Mataifa ya Afrika kwenye hatua ya makundi baada ya kushindwa kupata ushindi wowote huko Gabon. Algeria waliingia katika michuano hiyo wakipewa nafasi kubwa kufanya vyema haswa kutokana na kikosi chake kilichosheheni nyota kadhaa akiwemo mchezaji bora wa mwaka wa Afrika Riyad Mahrez. Hata hivyo, katika hali isiyotegemewa wamejikuta wakitolewa baada ya kung’ang’aniwa sare ya mabao 2-2 na vinara wa kundi B Senegal iliyohitimisha safari yao. Senegal sasa anatarajiwa kucheza na Cameroon katika hatua ya robo fainali Jumamosi hii huku mshindi wa pili kwenye kundi hilo Tunisia ambao waliigaragaza Zimbabwe kwa mabao 4-2, wao wakicheza na Burkina Faso.

No comments:

Post a Comment