Monday, January 23, 2017

AUBAMEYANG ALIA NA MAANDALIZI MABOVU KUFUATIA KUTOLEWA MAPEMA KWA WENYEJI GABON.

MSHAMBULIAJI wa kimataifa wa Gabon, Pierre-Emerick Aubameyang anaamini kutokuwa na maandalizi ya kutosha ndio kitu kilichochangia kuenguliwa mapema katika hatua ya makundi ya michuano ya mataifa ya Afrika. Gabon walikuwa wanatakiwa kuwafunga Cameroon jana ili waweze kusonga mbele lakini badala yake waliambulia sare ya bila kufungana. Aubameyang amesema ni jambo linalomkera kwasababu walikuwa na nafasi lakini anasikitika mambo hayakwenda kama walivyotarajia. Nyota huyo aliendelea kudai kuwa wamehuzunika lakini pia hawakupata muda wa kutosha wa kufanya maandalizi kwa ajili ya michuano hiyo. Burkina Faso walitinmga hatua hiyo wakiwa vinara wa kundi A wakifiatiwa na Cameroon waliomaliza katika nafasi ya pili.

No comments:

Post a Comment