Monday, January 23, 2017

ZIDANE ALIA NA MAJERUHI BAADA YA MODRIC NA MARCELO KUUMIA.

KLABU ya Real Madrid imethibitisha mapema leo kuwa nyota wake Luka Modric na Marcelo wote wamepata majeruhi ya msuli wa paja. Nyota hao walitolewa katika mchezo dhidi ya Malaga ambao Madrid walishinda mabao 2-1, ikiwa ni ushindi wao wa kwanza baada ya kupoteza mechi zao mbili zilizopita dhidi ya Sevilla na Celta Vigo. Hata hivyo ushindi huo umekuja kwa gharama baada ya nyota hao wawili kongeza idadi ya majeruhi katika kikosi hicho ambapo tayari inawajumuisha Gareth Bale, James Rodriquez, Dani Carvajal, Pepe, Danilo na Fabio Coentrao. Akizungumza na wanahabari Zidane amesema suala la majeruhi kidogo linamchanganya kwani wana mechi kubwa Jumatano ijayo. Madrid inakabiliwa na mchezo mgumu wa robo fainali wa mkondo wa pili wa Kombe la Mfalme dhidi ya Celta Vigo ambapo katika mchezo wa kwanza walipoteza kwa mabao 2-1.

No comments:

Post a Comment