Monday, January 23, 2017

COSTA ASABABISHA MAAFA KWA KIUNGO WA HULL CITY.

KIUNGO wa Hull City, Ryan Mason amefanyiwa upasuaji baada ya kuvunjika kwa fuvu la kichwa chake wakati wa mchezo wa Ligi Kuu dhidi ya Chelsea jana. Masom mwenye umri wa miaka 25, aligongana kwa kichwa na beki wa Chelsea Gary Cahill katika dakika ya 13 ya mchezo huo. Baada ya kutibiwa kwa dakika nane uwanjani, Mason aliwekewa mashine ya kumsaidia kupumua na kutolewa nje akiwa amebebwa kwenda machela kabla ya kukimbizwa hospitali moja kwa moja. Taarifa kutoka kwa klabu hiyo zimedai kuwa kwasasa kiungo huyo yuko katika hali nzuri na anategemewa kuendelea kubakia hospitali kwa siku chache zijazo. Mabao ya Diego Costa na Cahill yalitosha kuipa Chelsea ushindi wa mabao 2-0 na kuendelea kujiimarisha kileleni mwa msimamo wa wa ligi kwa tofauti ya alama nane.

No comments:

Post a Comment