Monday, January 23, 2017

WENGER AOMBA RADHI KWA VURUGU ALIZOFANYA.

MENEJA wa Arsenal, Arsene Wenger ameomba radhi kwa tabia mbovu aliyoonyesha mwishoni mwa mchezo dhidi ya Burnley jana, ambapo waliibuka na ushindi wa mabao 2-1. Wenger alionekana wazi akizozana na mwamuzi wa akiba aliyemuamuru kutoka uwanjani na kwenda jukwaani kwa kumsukuma. Meneja huyo alitolewa katika benchi lake la ufundi kwa tabia aliyoonyesha baada ya Burnley kupewa penati katika dakika za nyongeza. Wenger amesema anajutia kila kitu kwani alipaswa kunyamaza na kuzuia hisia, hivyo anaomba radhi kwa tukio hilo. Hata hivyo, meneja huyo aliendelea kudai kuwa hakupata nafasi ya kuomba radhi moja kwa mwamuzi huyo Anthony Taylor na kuna uwezekano wa kupata adhabu zaidi kutoka FA kwa tukio hilo.

No comments:

Post a Comment