Sunday, January 22, 2017

WENYEJI GABON WAAGA AFCON MAPEMA.

TIMU ya taifa ya Gabon imeaga michuano ya Mataifa ya Afrika jana na kuwa nchi ya tatu mwenyeji kutolewa katika hatua ya makundi. Gabon wakiongozwa na mshambuliaji wake nyota anayekipiga katika klabu ya Borussia Dortmund ya Ujerumani, waling’ang’aniwa sare ya bila kufungana na Cameroon ambao wametinga hatua ya robo fainali. Mara ya mwisho timu mwenyeji kutolewa katika hatua za mapema ilikuwa mwaka 1994 wakati Tunisia walipoaga michuano hiyo katika hatua makundi. Katika mchezo mwingine Burkina Faso walifanikiwa kutinga hatua ya robo fainali wakiwa vinara wa kundi A baada ya kuichapa Guinea Bissau kwa mabao 2-0.

No comments:

Post a Comment