Friday, January 20, 2017

DEPAY ATUA RASMI LYON.

KLABU ya Manchester United imemuuza rasmi winga wa kimataifa wa Uholanzi Memphis Depay kwenda klabu ya Lyon ya Ufaransa. Taarifa zinadai kuwa ada uhamisho huo ni paundi milioni 16 inayoweza kupanda mpaka paundi milioni 21.7 kama Lyon wakifuzu michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya na Depay akipewa mkataba mpya. United pia imekubaliana na Lyon kupewa kipaumbele kama klabu hiyo itaamua kumuuza mchezaji huyo. Depay mwenye umri wa miaka 22 amefunga mabao saba katika mechi 53 alizoichezea United toka ajiunge nao kwa kitita cha paundi milioni 25 akitokea PSV Eindhoven ya Uholanzi mei mwaka 2015.

No comments:

Post a Comment