Thursday, January 19, 2017

MAN UNITED YAIPITA REAL MADRID KWA KUINGIZA MAPATO MENGI ZAIDI.

KLABU ya Manchester United imetajwa kupata mapato makubwa zaidi kuliko klabu yeyote duniani msimu uliopita kwa mujibu ya taarifa iliyochapishwa na jarida la Deloitte. United imeipita Real Madrid ambayo imekuwa ikiongoza orodha hiyo kwa miaka 11, baada ya kuweka rekodi ya kupata mapato ya kiasi cha paundi milioni 515 wakati wa msimu wa 2015-2016. Klabu hiyo ya Ligi Kuu imeshuhudia mapato yake kibiashara yakiongezeka kwa paundi milioni 71. Hiyo inakuwa mara ya kwanza kwa United kuongoza orodha hiyo ya mwaka ya Deloitte Football Money League toka msimu wa 2003-2004. Madrid wamshuka mpaka nafasi ya tatu nyuma ya mahasimu wao Barcelona ambao wamebaki katika nafasi ya pili nao Bayern Munich na Manchester City zote zimepanda katika nafasi ya nne na tano ikiwa ni mara ya kwanza kupanda kwenye tano bora. Mabingwa wa Uingereza Leicester City wameingia katika orodha hiyo kwa mara ya kwanza wakishika nafasi ya 20 huku Arsenal, Chelsea, Liverpool na Tottenham Hotspurs zote zimebaki kwenye nafasi zao za saba, nane, tisa na 12.


No comments:

Post a Comment