Tuesday, January 31, 2017

MKWASA KATIBU MKUU MPYA YANGA.

KLABU ya Yanga, imemtangaza kocha wa zamani wa timu ya taifa, Taifa Stars, Charles Boniface Mkwasa kuwa Katibu Mkuu mpya wa klabu hiyo. Mkwasa ambaye kabla ya kuinoa Taifa Stars aliwahi kuwa kocha msaidizi wa Yanga, anachukua nafasi ya Baraka Deusdedit ambaye ametolewa na kupewa nafasi ya bwana fedha. Akizungumza mara baada ya kutangazwa kwa wanahabari na Makamu Mwenyekiti wa klabu hiyo Clement Sanga, Mkwasa amesema atajitahidi kufanya kazi kwa weledi wake wote kuhakikisha timu hiyo inafikia malengo waliyojiwekea. Mkwasa pia aliziasa klabu zingine kufuata nyayo za Yanga kwa kuteua viongozi ambao wanalifahamu soka kwa undani wake. Katika hatua nyingine Sanga aligusia suala la timu hiyo kugoma kucheza mechi ya kirafiki dhidi ya mabingwa wa Afrika Mamelodi Sundowns ya Afrika Kusini ambao wameweka kambi nchini kwa ajili ya kujiwinda na mechi yao Super Cup dhidi ya TP Mazembe ya Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo-DRC. Sanga amesema kikubwa kinachofanya wasikubali wito wa mechi hiyo ni kutokana na suala hilo kuja ghafla huku wakikabiliwa na mechi muhimu ya Ligi Kuu.

No comments:

Post a Comment