Tuesday, January 31, 2017

ADEBAYOR ATIMKIA UTURUKI.

MSHAMBULIAJI wa zamani wa klabu za Arsenal na Tottenham Hotspurs, Emmanuel Adebayor anatarajiwa kukamilisha uhamisho wake kwenda Basaksehir ya Istabul baada ya kukamilihs avipimo vya afya na klabu hiyo. Nyota huyo wa kimataifa wa Togo alikuwa bila timu toka alipoondoka Crystal Palace Juni mwaka 2016 na sasa anatarajiwa kusaini mkataba wa miezi 18 na klabu hiyo inayoshiriki Ligi Kuu ya Uturuki. Mapema leo Adebayor alituma picha katika ukurasa wake wa mtandao wa kijamii wa twitter akifanyiwa vipimo vya afya na nyingine akiwa amevaa jezi ya klabu hiyo. Adebayor alikuwa akifanya mazungumzo na Lyon, lakini inaripotiwa kuwa uhamisho wake ulikwama kutokana na ushiriki wake katika michuano ya Mataifa ya Afrika akiwa na Togo. Akizungumza na wanahabari Adebayor alikiri dili lake la kujiunga na Lyon lilishindikana kwasababu ya ushiriki wake katika michuano hiyo.

No comments:

Post a Comment