Tuesday, January 31, 2017

AFCON 2017: MAKOCHA WA ULAYA WAENDELEA KUTAMBA.


Duarte
MICHUANO ya Mataifa ya Afrika inayoendelea huko nchini Gabon imefikia hatua nusu fainali huku timu zilizofanikiwa kufika hatua hiyo zote zikiwa zinafundishwa na makocha wa kigeni kutoka bara la Ulaya. Baadhi ya timu zilizokuwa zikifundishwa na makocha wazawa akiwemo Callisto Pasuwa wa Zimbabwe, Baciro Cande wa Guinea Bissau, Florent Ibenge wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo-DRC na Aliou Cisse wa Senegal wote wakiwa wameshatolewa. Marehemu Stephen Keshi ndio kocha wa mwisho kupata mafanikio mwaka 2013 wakati Nigeria ilipotwaa taji la michuano hiyo huku kwa mwaka huu Ibenge na Cisse ndio makocha wazawa waliopata mafanikio kwa kuzifikisha timu zao robo fainali. Nguli wa soka wa zamani wa Cameroon, Rodger Milla amesema AFCON ni michuano migumu hivyo inahitaji makocha wa kiwango cha juu, na inafurahisha kuona makocha wazawa wakifanya vyema kiasi kwani hilo litawaongezea nafasi zaidi na pia kujifunza kutoka kwa wenzao wa Ulaya. Kocha wa Hector Cuper wa Misri, Avram Grant wa Ghana, Hugo Broos wa Cameroon na Paulo Duarte wa Burkina Faso ndio pekee walibakia katika michuano hiyo na wote wanatoka Ulaya.

No comments:

Post a Comment