Tuesday, January 31, 2017

N'ZONZI AJITIA KITANZI SEVILLA.

KIUNGO wa Sevilla, Steven N’Zonzi amesaini mkataba mpya ambao utamuweka klabu hapo mpaka Juni mwaka 2020. Nyota huyo wa kimataifa wa Ufaransa amekuwa akihusishwa na tetesi za kwenda Barcelona na Chelsea katika miezi ya karibuni lakini sasa amemaliza uvumi huko kwa kusaini mkataba mpya na Sevilla. Mkataba wake wa awali ulikuwa unamalizika mwishoni mwa msimu 2018-2019, lakini sasa amepewa mkataba zaidi baada ya kuonyesha kiwango bora. Taarifa za N’Zonzi kuongeza mkataba mpya zilitangazwa katika mtandao wa klabu hiyo huku kukiwa na uwezekano wa kuongezwa msimu mmoja zaidi. N’Zonzi alijiunga na Sevilla akitokea Stoke City Julai 2015.

No comments:

Post a Comment