Tuesday, January 31, 2017

LEVERKUSEN YANASA CHIPUKIZI WA GENK.

KLABU ya Bayer Leverkusen imekamilisha usajili wa winga chipukizi wa Genk anayetabiriwa kuja kung’aa sana siku za baadae, Leon Bailey. Chipukizi huyo wa kimataifa wa Jamaica amesaini mkataba wa miaka mitano na klabu hiyo ya Bundesliga. Bailey mwenye umri wa miaka 19 amekuwa akiwaniwa na vilabu kadhaa barani Ulaya huku Manchester United ikiwa mojawapo. Mwezi Novemba mwaka jana, Bailey aliweka wazi kuwa kama United wanamuhitaji na hawatamuhakikishia nafasi ya kucheza mara kwa mara atakaa kwenda huko. Liverpool pia waliwahi kuripotiwa kumuwania chipukizi huyo lakini nao walishindwa huku Ajax Amsterdam ikiwa klabu nyingine ya Ligi Kuu iliyokuwa ikimuwania.

No comments:

Post a Comment