Tuesday, January 31, 2017

PATO AKAMILISHA USAJILI WAKE CHINA.

MSHAMBULIAJI wa zamani wa Chelsea na AC Milan, Alexandre Pato amekuwa mchezaji wa hivi karibuni kwenda China kufuatia kujiunga na klabu ya Tianjin Quanjian. Pato mwenye umri wa miaka 27 amehamia China baada ya kuichezea kwa kipindi kifupi Villarreal ambako amefunga mabao sita katika mechi 24 alizocheza katika mashindano yote. Nyota huyo wa zamani wa kimataifa wa Brazil anajiunga na Tianjin ambayo inanolewa na beki nguli wa zamani wa Italia Fabio Canavaro na imepanda msimu huu katika Ligi Kuu ya nchi hiyo inayojulikana kama Chinese Super League. Pato alithibitisha taarifa hizo kupitia ukurasa wake wa mtandao wa kijamii wa twitter akidai kuwa anafurahia kujiunga na familia hiyo mpya. Pato aliibuka katika klabu ya Internacional na baadae Milan kabla ya majeruhi ya mara kwa mara kumzuia kung’aa kama ilivyotegemewa.

No comments:

Post a Comment