Tuesday, January 31, 2017

AFCON 2017: WACHEZAJI CAMEROON WALILIA POSHO ZAO.

WACHEZAJI wa timu ya taifa ya Cameroon waligoma kufanya mazoezi jana huko Gabon kufuatia sakata la kutopewa posho zao. Kikosi hicho kinachojulikana kama Indomitable Lions kinataka posho hiyo iliyotokana na kiwango bora walichoonyesha katika mchezo wa robo fainali na kuiondoa Senegal iliyokuwa ikipewa nafasi kubwa ya kufanya vizuri, kwa changamoto ya mikwaju ya penati 5-4. Taarifa kutoka katika kambi ya timu hiyo zinadai kuwa wachezaji hao wanaonolewa na kocha Hugo Broos wanalidai Shirikisho la Soka la Cameroon fedha zao za bakshishi kwa kufanikiwa kwao kutinga hatua ya nusu fainali. Wachezaji hao wanataka serikali kuingilia kati suala hilo na kulipwa fedha zao kabla ya kuanza tena mazoezi kwa ajili ya mchezo wao wa nusu fainali dhidi ya Ghana Alhamisi hii.

No comments:

Post a Comment