Tuesday, January 17, 2017

MMILIKI WA TIANJIN AKIRI KUMUWANIA COSTA.

MMILIKI wa klabu ya Tianjin Quanjian, Shu Tuhui amethibitisha kuwa alikuwa na mipango ya kuwasajili Diego Costa, Karim Benzema, Edinson Cavani na Radamel Falcao mpaka pale Chama cha Soka cha China-CFA kilipobadili sheria ya idadi ya wachezaji wa kigeni. Wakiwa tayari wameshamnasa nyota wa kimataifa wa Ubelgiji Axel Witsel, klabu hiyo inayonolewa na beki wa zamani wa Real Madrid na Juventus Fabio Canavaro, imekuwa ikihusishwa na tetesi za kutaka kuwasajili Costa na wenzake. Yuhui amebainisha kuwa Tianjin ilikuwa katika mazungumzo na Costa, Benzema, Cavani na Falcao kabla ya CFA hawajatangaza sheria mpya ambapo timu zinazoshiriki Ligi Kuu ya China zitalazimika kutumia wachezaji watatu pekee wa kigeni kwa mchezo. Akihojiwa Yuhui amesema klabu yao ilikuwa na mipango mikubwa ya uwekezaji kwa ajili ya msimu mpya lakini wamebanwa na sheria hiyo mpya.

No comments:

Post a Comment