Tuesday, January 17, 2017

VAN GAAL AAMUA KUSTAAFU RASMI SOKA.

KOCHA wa zamani wa timu ya taifa ya Uholanzi na klabu ya Manchester United, Louis van Gaal ametangaza kustaafu rasmi kibarua hicho baada ya kudumu kwa kipindi cha miaka 26. Van Gaal mwenye umri wa miaka 65 amekuwa bila kazi toka alipotimuliwa na United saa chache baada ya kushinda taji la Kombe la FA Mei mwaka jana. Van Gaal amesema mara ya kwanza alifikiria kuwa atasimama kwa muda lakini baada ya kufikiria kwa muda anadhani imetosha na hataweza tena kurejea kufundisha soka. Mbali na United Van Gaal pia amewahi kuzinoa klabu za Ajax Amsterdam, Barcelona, Bayern Munich na AZ. Van Gaal alitangaza uamuzi huo jana baada ya kupokea tuzo ya mafanikio ya maisha kutoka kwa serikali ya Uholanzi kutokana na mchango wake mkubwa katika soka.

Mataji aliyowahi kushinda.
National titles: Ajax (1993-94, 1994-95, 1995-96), Barcelona (1997-98, 1998-99), AZ Alkmaar (2008-09), Bayern Munich (2009-10)
Champions League: Ajax (1994-95)
Uefa Cup: Ajax (1991-92)
FA Cup: Manchester United (2015-16)

No comments:

Post a Comment