Monday, January 16, 2017

CHINA YAAMUA KUPUNGUZA IDADI YA WACHEZAJI WA KIGENI.

KLABU zinazoshiriki Ligi Kuu ya China zitaruhusiwa kutumia wachezaji watatu pekee wa kigeni katika mchezo katika msimu wao ujao wa ligi ambao utaanza Machi mwaka huu. Sheria hiyo ya mabadiliko imepunguza idadi ya wachezaji wa kigeni wanaohitajika hatua ambayo itapunguza wimbi la kusajiliwa wachezaji kwa fedha nyingi kutoka Ulaya. Mshambuliaji wa Chelsea Diego Costa amekuwa akihusishwa na tetesi za kutimkia China huku taarifa zikidai atakuwa akilipwa paundi milioni 30 kwa mwaka kama dili hilo likikamilika. Klabu ya Tianjin Quanjiani ambayo mapema mwezi huu ilimsajili nyota wa kimataifa wa Ubelgiji Axel Witsel kwa mshahara wa paundi milioni 15 kwa mwaka ndio wanaidaiwa kumuwania Costa. Taarifa za kupunguzwa kwa idadi ya wachezaji wa kigeni itaigusa moja kwa moja klabu ya Shanghai Shenhua ambayo ina wachezaji sita wa kigeni wakiwemo Carlos Tevez, mshambuliaji wa zamani wa Chelsea Demba Ban a mshambulaiji wa zamani wa Newcastle Obafemi Martins.

No comments:

Post a Comment