Monday, January 16, 2017

ROMA WAMUWANIA CHIPUKIZI WA CHELSEA.

MENEJA wa AS Roma, Luciano Spalletti amethibitisha klabu hiyo kumuwania chipukizi wa Chelsea Charly Musonda katika kipindi hiki cha usajili wa Januari. Nyota huyo wa kimataifa wa Ubelgiji mwenye umri wa miaka 20 alikatishwa mkataba wake wa mkopo katika klabu ya Real Betis huku meneja wa Chelsea Antonio Conte akisisitiza kuwa anaweza kumpa nafasi katika kikosi chake cha kwanza. Lakini Spalletti amebainisha kuwa anataka sana kumleta Musonga Stadio Olimpico kabla ya mwishoni mwa mwezi huu. Meneja huyo raia wa Italia pia anataka kumuwania winga wa West Ham United Sofiene Feghouli ambaye ameshindwa kung’aa katika klabu hiyo toka asajiliwe akitokea Valencia kiangazi mwaka jana.

No comments:

Post a Comment