Monday, January 16, 2017

ROBBEN AFUATA NYAYO ZA RIBERY BAYERN.

WINGA mahiri wa Bayern Munich, Arjen Robben amefikia makubaliano na klabu hiyo ya kuongeza mkataba mpaka ambao utamuweka hapo mpaka Juni mwaka 2018. Nyota huyo wa kimataifa wa Uholanzi mkataba wake wa sasa unamalizika mwishoni mwa msimu huu, lakini ameamua kuongeza mkataba wa mwaka mmoja zaidi. Robben alijiunga na Bayern akitokea Real Madrid Agosti mwaka 2009 na toka wakati amekuwa mchezaji muhimu katika kikosi cha timu hiyo. Winga huyo mwenye umri wa miaka 32 ameichezea Bayern zaidi ya mechi 200, na kushinda mataji matano ya Bundesliga, manne ya DFB Pokal, moja la Ligi ya Mabingwa Ulaya na Klabu Bingwa Dunia. Robben amefuata nyayo za winga mwenzake Franck Ribery ambaye naye alisaini mkataba wa mwaka mmoja zaidi Novemba mwaka jana.

No comments:

Post a Comment